Monday, 11 November 2013

Jamaa atolewa kaburini akiwa hai



Hii imetokea huko Brazili ambapo jamaa mmoja ametolewa kaburini akiwa hai baada ya kuwa amezikwa kwa bahati mbaya akiwa bado mzima. Tukio hili limetokea katika kitongoji cha Ferraz de Vasconcelos mjini Sao Paulo ambapo mpaka sasa jamaa huyo anaendelea kutibiwa hospitalini.

Jamaa huyo aliezikwa akiwa hai alipataa bahati hiyo ya kuokolewa baada ya mwanamke mmoja muombelezaji aliposikia kelele zikitokea ndani ya kaburi.


Inaarifiwa kuwa mwanamke huyo muombolezaji  aliwataarifu polisi juu ya sauti aliyoisikia kutokea ndani ya kaburi lakini hawakumwamini na iliwabidi wamtafute mtunza makaburi ili aweze kuthibitisha habari hizo.

Picha za video zinamuonesha jamaa huyo akitolewa toka kaburini na akiwa amelezwa katika majani huku hajitambui.


Chanzo

No comments:

Post a Comment