Saturday, 16 March 2024

Treni lazinduliwa kwa "tambiko" - India


Shirika la CRRC (China Railway Rolling Stock Corporation) Nanjing Puzhen, kwa ubia na Titagarh Rail Systems wametengeneza na kukabidhi treni ya kwanza ya metro isiyo na rubani kwa jiji la Bangalore, India.

Treni hiyo ni ya kwanza katika treni zinazoundwa kwa ajili ya Bangalore Metro Yellow Line, inayotarajiwa kufunguliwa majira ya joto ya 2024.

Jambo moja lililofanyika wakati wa uzinduzi wa treni hii ni tukio la "tambiko" ambapo wanaonekana maofisa wakivunja na kwamwaga "vitu" mbele ya treni hiyo na huku treni likiwa limepambwa kwa maua.

Hayo ndio mambo ya Walimwengu katika Ulimwengu.😂

Fuatilia mitandao yetu ya kijamii; instagram, youtube, twitter, facebook, tiktok, ili kupata taarifa mbalimbali kwa haraaka kadri zinavyotokea                                                 

Tuesday, 18 February 2014

Usimtegemee sana mwanadamu katika maisha yako.

Katika kijiji cha Matare wilaya ya Mugumu Serengeti, bwana Wambura alikamatwa kwa kesi ya kusingiziwa na kuhukumiwa kwenda jela miaka mitatu, huku nyuma akiacha mke na watoto wanne waliokuwa wanasoma. Hukumu hiyo ilimtesa sana kichwa chake, alitamani kila mtu anayemhisi kuwa ana makosa aingie katika moyo wake na kuupata ukweli. 

Alilia na umaskini wake, labda angepata wakili mzuri angeweza kumtetea, kumkosa wakili kukahalalisha kifungo hicho!! Alikwenda gerezani huku akiumia sana rohoni.

Aliyaanza maisha mapya kwa shida sana, akawa mnyonge kila mara na mwili ukapoteza afya kiujumla. Huko gerezani alifanikiwa kupata rafiki aliyekuwa na cheo ama jukumu la uzikaji wa wafungwa hasahasa ambao hawakuwa na ndugu ama ambao ndugu zao huwa hawajitokezi pale gerezani.

Mzikaji alijaribu sana kumtia nguvu Wambura na kumwaminisha kuwa hiyo ilikuwa hatua tu ya maisha anapaswa kuizoea na siku moja ukweli utajulikana tu! Bwana Wambura maneno ya mzikaji hayakumuingia kabisa...alizidi kunyong’onyea. “Siwezi kuvumilia kukaa gerezani miaka mitatu…..kama unajali kilio changu nisaidie nitoroke kwa namna yoyote ile ndugu yangu!!” Wambura alimsihi mzikaji.

SIKU MOJA mzikaji akamwambia Wambura kuwa msaada umepatikana. Lakini yataka moyo!! “Nipo tayari kwa lolote ilimradi tu nitoke humu!!” alijibu kwa msisitizo huku akimtegea sikio mzikaji. “Msaada pekee wa kukutorosha humu ndani ni kwa njia ya jeneza… yaani mfungwa akifa mimi nakuunganisha naye kwenye jenerza…..” akashusha pumzi kisha akaendelea “Wewe ukisikia kengere ya msiba, njoo mara moja kwenye chumba cha maiti, utakuta tayari sanduku liko katikati ya chumba linakuwa halijafungwa, funua kifunioko ingia ndani yake ulale pembeni ya maiti kwani sanduku huwa kubwa la kutosha kila aina ya maiti na hata miili miwili inaingia. Kisha nitakuja na kulipigilia misumari. Baada ya muda tutalipakia kwenye gari na kutoka kwenda nje ya gereza makaburini nikiongozana na baadhi ya wafungwa na maaskari magereza. Tutakuzika huko lakini baada ya dakika 20 hadi 30 nitarudi kukufukua. Hautaweza kushindwa kupumua kwa dakika hizo, utatoka ukiwa huru.” 

JAPOKUWA wazo lilikuwa zuri lakini lilimtisha sana Wambura. Hata hivyo akaona afadhali afanye hivyo kuliko kukaa gerezani miaka mitatu bila kosa.

Siku moja akasikia kengere ya msiba. Akafanya kama alivyoelekezwa na mzikaji. Akaenda na kuingia chumba cha maiti. Kweli akalikuta sanduku, akiwa na hofu kuu akaingia na kulala pembeni ya maiti iliyokuwepo. Mara akasikia mtu ameingia na kulipigilia msumari sanduku. Muda mfupi baadaye sanduku likainuliwa na kuwekwa kwenye gari. Gari ikatoka nje ya gereza hadi makaburini. Sanduku likashushwa na kuwekwa kaburini na kuanza kufukiwa. Wambura alijitahidi sana kuvumilia japo hofu ilizidi kutanda. Alimtegemea sana mzikaji na alianza kumuona mkombozi wa maisha yake. Kama alivyoambiwa, akasubiri dakika kumi, ishirini.. zikapita kimya!! Dakika thelathini kimya. Joto nalo likazidi kuongezeka. “Nitavumilia hadi afike…” alijisemea kisha akajiongezea kauli ya ujasiri. “Kama nilitakiwa kuishi gerezani miaka mitatu kivipi dakika kadhaa za hapa kaburini” 

KWA kuwa alishakaa gerezani kwa muda kiasi akatamani kujua aliyekufa ni nani… ni kwewli aliogopa kuitazama maiti lakini aliona kama inatisha zaidi ikiwa imefunikwa vile kuliko ikiwa wazi. Akaifunua upande wa usoni… Kwa kuwa kulikuwa na giza nene alikodoa sana macho kuitazama. LAHAULA!!! MACHO YAKAKUTANA NA SURA YA MZIKAJI!!! MZIKAJI ALIKUWA AMEKUFA NA AMEZIKWA NA AHADI ZAKE ZA UKOMBOZI!! 


FUNZO:: Usimtegemee sana mwanadamu katika maisha yako, kwanza ni dhambi!! Pili mwanadamu anakumbana na vikwazo kama unavyokumbana navyo wewe hadi kumwendea yeye. Hivyo kumpatia maisha yako ni kuzidi kuyaweka hatarini zaidi!! Umeonewa umesingiziwa unanyanyaswa….. mwachie Mungu afanye maamuzi… 

Haya mzikaji aliyetegemea atamfukua naye ni maiti…… tazama mateso atakayoyapata hadi kufa kwake….. Bila shaka atatamani kurudi gerezani kwa miaka mingine kumi lakini haitawezekana tena!!!

MCHAWI WA UNGO ADONDOKA, AGEUKA KUKU


HALI ya taharuki iliyoambatana na imani za kishirikina iligubika Jiji la Arusha kufuatia mwanamke ambaye hakufahamika jina kudondoka na ungo wa kishirikina asubuhi ya Ijumaa iliyopita kisha ghafla kubadilika  kuwa kuku mweupe mwenye mayai ndani ya ungo, Uwazi limeona mengi.
Kuku aliyebadilika kutoka hali ya ubinadamu akiwa katika ungo.
Mamia ya wananchi katika eneo la Kimandolu kando ya Barabara ya Arusha- Moshi walimiminika kushuhudia tukio hilo lililojiri saa tatu asubuhi.
Akizungumza na Uwazi, shuhuda mmoja wa tukio hilo ambaye ni dereva wa bodaboda, Martin Mbise alisema:
“Nilikuwa kwenye shughuli zangu za kila siku, ghafla niliona kitu kipana kikidondokea kwenye huu mtaro, ndani yake nikamwona mtu amekaa akiwa uchi wa mnyama.


“Wengi tuliamua kusogelea eneo la tukio, lakini kabla hatujakifika, mtu huyo alitoweka, badala yake mle mwenye ungo  mkawa na kuku mweupe na mayai zaidi ya kumi, tulishangaa sana:
Mbise alisema hali hiyo ilidumi kwa saa mbili na nusu, ndipo wananchi hao wakaamua kumchoma moto kuku huyo baada ya kumuua na kuyavunja mayai.

Hata hivyo, alisema haikuwa rahisi kuku huyo kuungua licha ya kumwagiwa mafuta ya taa na petroli na wakachukua uamuzi wa kumkatakata na kugawana nyama yake huku baadhi
yao wakikimbia hovyo na kulaani tukio hilo.

Baadhi ya wakazi wa eneo hilo walisema tukio hilo ni laana na anapaswa kuitwa mtumishi wa Mungu kwa ajili ya kukemea pepo mchafu kwa maombi ya kiroho wakiamini mchawi huyo alikuwa ana lengo la kuwadhuru.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, ACP Lebaratus Sabas hakuweza kupatikana kuzungumzia tukio hilo, lakini baadhi ya maafande waliofika katika eneo hilo walithibitisha.

CHANZO: http://www.globalpublishers.info/

Thursday, 14 November 2013

Wanandoa wawili huko China wauza watoto wao ili kulipia iPhones na Viatu.

Katika hali ya kushangaza na kustaajabisha, familia ya wanandoa wawili huko Shanghai imeshitakiwa kwa tuhuma za  kuwauza watoto wao watatu wa kuwazaa wenyewe ili kuweza kumudu gharama za kulipia iPhones, Komputa na viatu vya gharama ya juu.

Mamlaka za nchini China zinaripoti kuwa, Mume na Mke wanaojulikana kwa majina ya Teng na Zhang, wote wakikadiriwa kuwa na umri wa miaka 30, wanakabiliwa na mashitaka kadhaa ya kusafirisha wanawake na watoto. Mume yupo rumande na mkewe amepata dhamana.

Polisi katika mji wa Shanghai walianza kuchunguza mienendo yawanandoa hao mwezi Mei mara baada ya kupokea taarifa kutoka kwa raia wema kuwa wanandoa hao walitumia mtandao wa QQ kuweka tangazo la kumuuza binti yao mchanga. Mtandao huo ni maarufu huko China kwa kupelekeana ujumbe mfupi. Polisi waliwapata wanandoa hao baada ya kufuatilia anuani (IP address) ya Komputa yao kupitia tangazo hilo.

Baada ya Polisi kuwakamata, wanandoa hao walikiri kuwauza watoto wao wachanga,watatu , katika kipindi cha miaka ya karibuni kwa jumla ya dola za kimarekani 13,000. 

Walimuuza mtoto wao wa kwanza mwaka 2008, wapili mwaka 2011 na watatu (wa kike) mwaka huu. Mamlaka zimefanikiwa kumpata mtoto huyo wa kike na sasa zinaendelea kuwatafuta wengine wawili.

Majirani wamewaeleza polisi kuwa familia hiyo bado inaishi na watoto wao wengine wawili walio na umri wa miaka 6 na 9. Majirani pia walisema kila mara Mke alionekana mjamzito lakini vichanga havikuonekana muda mfupi tu baada ya kuzaliwa.

Baada ya kufuatilia taarifa za kadi ya benki ya na miamala ya kibenki ya Mke polisi waligundua kuwa wanandoa hao walitumia fedha zao zote za mauzo ya watoto wao kwa kununulia simu aina za iPhones na viatu vya anasa. Pia walinunua komputa kadhaa ambapo polisi walifanikiwa kukuta vitu hivyo vyote nyumbani kwa wanandoa hao.

Wanandoa walidai kuwa waliwauza watoto wao kwa matumaini kuwa watoto hao watapata maisha bora zaidi na pia watu walijitolea kuwapa fedha ingawa wao hawakudai malipo yeyote kutoka kwa watu waliochukua watoto hao.

Hata hivyo taarifa zinadai kuwa suala la kuuza watoto nchini China ni limekuwa ni tatizo kwa miaka kadhaa iliyopita. Mwaka 2011 Wizara ya ulinzi wa uma ilitangaza kusambaratisha mitandao miwili ya kuuza na kusafirisha watoto na kuwaokoa watoto wachanga wapatao 29 katika jimbo la mashariki la Shandong. Watoto hao waliuzwa na wazazi wao wa kuwazaa.

Chanzo: CNN


Aliyemuua mtoto wa miaka mitatu aomba asinyongwe, achangie viungo kwanza.

Hukumu ya kunyongwa kwa Ronald Philllips aliyepatikana na hatia ya kumuua mtoto wa miaka mitatu katika jimbo la Ohio nchini Marekan imeahirishwa kutokana na mshitakiwa huyo kuomba kuchangia baadhi ya viungo vyake vya mwili zikiwemo figo ili kunusuru uhai wa mama anayeumwa.

Ronald Phillips alitarajiwa kunyongwa Alhamis kwa njia ya sindano ya sumu baada ya kupatiakana na hatia ya kumuua mtoto wa kike mwenye umri wa miaka mitatu mwaka 1993.

Gavana wa jimbo la Ohio John Kasich amesema kama ombi hilo la mshitakiwa litasaidia kuokoa uhai wa mtu mwingine basi na likubalike, lakini litakuwa jambo geni kuahirishwa kwa adhabu iliyokwisha kupitishwa japo kuwa madaktari wanapaswa kuthibitisha.

Phillips mwenye umri wa miaka 40 alihukumiwa kifo kutokana na makosa ya ubakaji na mauaji ya binti wa rafiki yake wa kike Sheila Marie Evans.

Dawa ya sumu iliyotarajiwa kutumika kumuua Phillips ni aina ya midazolam na hydromorphone, mchanganyiko wa dawa ambayo ingetumika kwa mara ya kwanza nchini Marekani kunyonga watu
Jimbo la Ohio liliamua kutumia mchanganyiko wa dawa hii kwa sababu haikuwa na kiasi cha kutosha cha dawa ya kawaida inayotumika kunyongea watu ijulikanayo kama pentobarbital.

Mama mzazi wa Phillips amekuwa akisumbuliwa na maradhi ya figo na dada yake Phillips pia anasumbuliwa na maradhi ya moyo ambapo anasema anahitaji kutoa viungo vyake haraka iwezekanavyo. 


Chanzo: BBC

Je umechoshwa na foleni za benki? Tazama ubunifu huu.

Kama umechoshwa kukaa katika misururu mirefu ya benki ukisubiri kuhudumiwa, ubunifu huu hapa katika picha waweza kusaidia. Je njia hii yaweza fanikiwa hapa bongo?


Siku njema!

Wednesday, 13 November 2013

Shehena kubwa ya meno ya tembo imekamatwa katika bandari ya Zanzibar.

Shehena kubwa ya pembe za tembo ikiwa na vipande 1,021 na uzito wa kilo 2,915  ambayo haijawahi kukamatwa nchini imenaswa  katika bandari ya Zanzibar huku ikishuhudiwa na mawaziri wa serikali zote mbili wakiongozwa na waziri wa mali asili na utalii Mhe Khamis Kagasheki.

Shehena hiyo iliyokuwa tayari kusafirishwa kuelekea Philiphine ilikuwa katika magunia 98 yaliyochanganywa na magunia mengine ambayo yalikuwa yamefungwa pamoja na baadhi ya vitu vya baharini yalikuwa tayari yameshawekwa ndani ya kontena la futi 40 tayari kwa kusafirishwa kwenda Philiphne yakiwa katika hatua za mwisho za mamlaka husika za bandarini.

Wakiongea na wandishi wa habari katika bandari ya Zanzibar waziri wa nchi afisi ya rais utawala bora na idara maalum Mhe Haji Omar Kheri amesema hii ni janga kubwa la nchi na serikali kamwe haitokubali  kuona wahusika wanaanchiwa na kuahidi sheria kufanya kazi yake ,kwa upande wake waziri Kagasheki ambaye aliwisili Zanzibar asubuhii kushuhudia shehena hiyo amesema ni lazima mtandao utokomezwe kwani utamaliza tembo wa nchii hii na kuipoteza rasilimali ya nchi.

Kwa upande wake kamishna wa jeshi la polisi Zanzibar CP Mussa Ali Mussa  amesema polisi imekamata watu wawili wazalendo na inaendelea kuwahoji na kufanya upekuzi nje ya bandari pamoja kwamba  taarifa zinaonyesha kuwa mzigo huo ni wa raia wa China.
 
 
Chanzo: ITV