Saturday, 16 March 2024

Treni lazinduliwa kwa "tambiko" - India


Shirika la CRRC (China Railway Rolling Stock Corporation) Nanjing Puzhen, kwa ubia na Titagarh Rail Systems wametengeneza na kukabidhi treni ya kwanza ya metro isiyo na rubani kwa jiji la Bangalore, India.

Treni hiyo ni ya kwanza katika treni zinazoundwa kwa ajili ya Bangalore Metro Yellow Line, inayotarajiwa kufunguliwa majira ya joto ya 2024.

Jambo moja lililofanyika wakati wa uzinduzi wa treni hii ni tukio la "tambiko" ambapo wanaonekana maofisa wakivunja na kwamwaga "vitu" mbele ya treni hiyo na huku treni likiwa limepambwa kwa maua.

Hayo ndio mambo ya Walimwengu katika Ulimwengu.😂

Fuatilia mitandao yetu ya kijamii; instagram, youtube, twitter, facebook, tiktok, ili kupata taarifa mbalimbali kwa haraaka kadri zinavyotokea